Vyombo vya Habari Vitumike Kuhamasisha Zoezi la Sensa -
Baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya Taifa ya Sensa kwa upande wa Zanzibar wakiendelea na Kikao chao Mjini Dodoma chini ya Mwenyekiti wa Kikao hicho Waziri Mkuu Mh. Mizengo Pinda.
Mwenyekiti wa Kamati ya Taifa ya Sensa Waziri Mkuu Mh. Mizengo Pinda akiwa na Mwenyekiti Mwenza Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Bazlozi Seif wakikiendesha Kikao cha Tatu cha Kamati hiyo katika Ukumbi wa Wizara inayosimamia Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mjini Dodoma.
Wajumbe wa Kamati ya Sensa upande wa Tanzania Bara wakiwa makini kuchangia Taarifa mbali mbali zilizowasilishwa kwenye Kikao hicho katika Ukumbi wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mjini Dodoma.
Na Othman Khamis Ame
Vyombo vya Habari Nchini bado vinapaswa kutumiwa Kisayansi katika
kutoa Elimu juu ya uhamasishaji wa umuhimu wa Zoezi la Sensa ya Watu na
Makaazi inayotarajiwa kufanyika Nchini kote Usiku wa Kuamkia Tarehe 26
Agosti mwaka 2012.
Ushauri huo umetolewa na Wajumbe wa Kamati ya Taifa ya Sensa ya Watu
na Makaazi katika Kikao chao cha Tatu kilichofanyika kwenye ukumbi wa
Mikutano wa Wizara ya Nchi Ofisi ya Waziri MkuuTawala za Mikoa na
Serikali za Mitaa.
Kikao hicho kilichoshirikisha Wajumbe wa Pande zote mbili za Jamuhuri
ya Muungano wa Tanzania ambao ni Mawaziri na Watendaji wa Kamati ya
Sensa kiliongozwa na Mwenyekiti wake Waziri Mkuu Mh. Mizengo Pinda
akiwa na Mwenyekiti Mwenza Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi
Seif Ali Iddi.
Wajumbe hao walisema baadhi ya vyombo vya Habari Watendaji wake
hawajawa na Uzalendo katika utowaji wa Elimu ya Sensa na badala yake
hutumia njia ya kupotosha.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Fedha, Uchumi na Mipango ya Maendeleo
Zanzibar Mh. Omar Yussuf Mzee alisisitiza kwamba Wana Habari ni vyema
wakawaongoza Wananchi hasa Vijijini katika kuwapatia Elimu hii.
Alishauri kutumiwa zaidi Redio za Jamii pamoja na Zile za masafa mafupi
{ yaani F.M. } katika kutoa Ujumbe wa Elimu ya Sensa kwa vile zimekuwa
na wasikilizaji wengi zaidi.
Kwa upande wake Waziri wa Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo
Zanzibar Mh. Said Ali Mbarouk ambaye ni Mjumbe Mpya katika Kamati hiyo
kufuatia mabadiliko ya Uteuzi wa Rais wa Zanzibar ya hivi karibuni
aliomba Vyombo vya Habari viwezeshwe zaidi ili kuwa na Uwezo wa kufanya
vipindi mbali mbali vya uhamasishaji Jami.
Mh. Said alisema mfumo na Taratibu za kuvitumia vyombo hivyo ni muhimu
na wa msingi ikizingatia kwamba asilimia kubwa ya Jamii hivi sasa
hutumia vyombo vya Habari katika kupata Elimu na Habari mbali mbali.
Waziri anayeshughulikia Ajira, Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi na
Ushirika Mh. Haroun Ali Suleiman alitoa wazo la kutumiwa kwa Wanafunzi
wa Skuli za Sekondari katika kufikisha ujmbe na Taaluma ya Sensa kwa
Jamii kwenye Maeneo yao.
Waziri Haroun alisema hatua hiyo inafaa kwenda sambamba na
ushirikishwaji wa Watu Maarufu , Waheshimiwa pamoja na Machifu katika
kusambaza Elimu hiyo muhimu kwa Taifa.
Akitoa baadhi ya ufafanuzi wa hoja ya baadhi ya wajumbe wa Kikao hicho
Kamishna wa Sensa Mh. Amina Mrisho Said alisema Kamati hiyo inapendelea
kuwa na Maswali machache kwenye zoezi la hesabu ya Watu na Makaazi.
Mh. Amina Mrisho alisema hatua hii hupunguza matumizi yasiyo ya lazima
kigezo cha Takwimu ambacho hutumiwa pia na Umoja wa Mataifa kwa
kuzitaka Nchi Wanachama wa Umoja huo kutumia mfumo huo.
Katika Nasaha zake Mwenyekiti wa Kamati ya Taifa ya Sensa Waziri Mkuu
wa Serikali ya Jamuhuri yha Muungano wa Tanzania Mh. Mizengo Pinda
ameshauri kutumiwa Ziara za Viongozi Wilayani na Mikoani katika
kupeleka Elimu na Ujumbe wa Sensa.
Mh. Pinda alieleza kuwa kutumiwa kwa utaratibu huo kutawezesha
kufikisha kwa haraka Taaluma hiyo kwa vile ziara hizo hukusanyisha
Wananchi walio wengi.
No comments:
Post a Comment