Alexander 2nd Great

Monday, October 29, 2012

Vigogo 10 wahusishwa mabilioni ya Uswisi
     Mheshimiwa Zitto Kabwe

mwanzo Habari kitaifa kitaifa Vigogo 10 wahusishwa mabilioni ya Uswisi Share bookmark Print Email Email this article to a friend Friend's Email Address Your Email Message Submit Cancel Rating Mheshimiwa Zitto Kabwe By Boniface Meena (email the author) Email this article to a friend Friend's Email Address Your Email Message Submit Cancel Posted Monday, October 29 2012 at 07:57 In Summary ZITTO ASISITIZA NYARAKA ZIPO, DK HOSEAH NDIYE ANAYEZIZUIA SHARE THIS STORY VIGOGO 10 wametajwa kuhusika katika kashfa ya kuficha Sh303.7 bilioni katika benki mbalimbali nchini Uswisi. Katika orodha hiyo inadaiwa kuwa yupo kiongozi mmoja mwandamizi mstaafu, maofisa watatu wastaafu wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), mawaziri wastaafu ambao baadhi yao bado ni wabunge na aliyewahi kuwa kiongozi mwandamizi wa Benki Kuu Tanzania (BoT). Majina hayo ambayo mwandishi wetu amefanikiwa kuyaona, yamo katika orodha ya mchunguzi mmoja wa kimataifa wa masuala ya ufisadi (jina tunalo). Juzi, Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe alimshukia Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Dk Edward Hoseah akimtuhumu kuandika barua Uswisi akisema Tanzania haina masilahi na mabilioni ya fedha yaliyofichwa katika benki zilizopo nchini humo. Hata hivyo, Dk Hoseah alikanusha madai hayo akisema hajawahi kufanya hivyo. Akizungumza jana Zitto alisisitiza kauli yake akisema: “Sijawahi kumsema Dk Hoseah kwa lolote, kwa nini leo nimsingizie? Yeye mwenyewe anajua ushirikiano niliompa wakati wabunge wanapinga yeye asichunguze malipo ya posho mara mbili kwa wabunge.” “Nilisimama kidete kusema Takukuru wapo sahihi na mimi nilikwenda mwenyewe kwao kuhojiwa na kuagiza wajumbe wa kamati yangu (Kamati ya Bunge ya Mashirika ya Umma), waende kuhojiwa. Spika aliyestaafu (Samuel Sitta) akaizima kashfa ya wabunge kupokea posho mara mbilimbili. Mwulizeni amesahau? Sasa leo nimzushie ili iwe nini?.” Alisema orodha ya Watanzania wenye fedha huko Uswisi, ipo na ameiona na nyaraka zinaweza kutolewa kwa taasisi za Serikali tu. “Dk Hoseah kazuia nyaraka hizo. Akitaka nimwonyeshe mtu anayeweza kutoa nyaraka hizo, nipo tayari isipokuwa aahidi kuiweka wazi,” alisema Zitto. Alisema katika orodha ambayo Waziri wa Fedha wa Ufaransa anayo, kuna Watanzania lakini akaituhumu Serikali akisema haitaki kufuata njia halali za kupata orodha hiyo kwa kuwa viongozi wengi na wafanyabiashara wakubwa wana akaunti katika benki za Uswisi. Juni 26, mwaka huu gazeti hili lilichapisha habari kuhusu utoroshwaji wa fedha hizo na kueleza kuwa Polisi wa Kimataifa (Interpol) nchini kwa kushirikiana na Takukuru inachunguza suala hilo. Kiasi hicho cha fedha kimedaiwa kuingizwa katika akaunti za Watanzania na kampuni moja ya uchimbaji mafuta na kampuni kadhaa za uchimbaji madini ambazo zinafanya kazi Tanzania. Chanzo hicho kiliongeza kwamba kiasi hicho cha fedha kipo katika akaunti sita tofauti zinazomilikiwa na Watanzania wakiwamo wanasiasa wakubwa. Hata hivyo, chanzo hicho kilieleza kuwa tangu akaunti hizo zifunguliwe, wamiliki wake halali hawajawahi kuingiza hata shilingi. “Uchunguzi wetu unaonyesha kuwa fedha hizo zipo katika akaunti sita tofauti ambazo zinamilikiwa na wanasiasa wakubwa nchini na wenzetu wa Uswisi wameeleza fedha hizo zimeingizwa na kampuni kadhaa ambazo zinahusika na mafuta pamoja na madini hapa nchini,” kilidokeza chanzo hicho. Kugundulika kwa kiasi hicho cha fedha katika benki za Uswisi ni kutokana na ripoti ya Benki ya Taifa ya Uswisi (SNB) iliyotolewa mwaka huu.

Friday, June 22, 2012

MAREKANI KUKIMBIA MBIO ZA MT. KILI MARATHON




Mcheza sinema maarufu duniani kutoka nchini Marekani Deidre Lorenz atakimbia mbio za kila mwaka za Mount Kilimanjaro Marathon zinazoanza kutimua vumbi kuanzia tarehe 24 Juni mwaka huu kutoka Moshi Club mjini Moshi.
Mbio hizi zilizoanzishwa na mama Marie France kutoka katika mji wa Bethesda, Maryland nchini Marekani mwaka 1991 ni mbio zinazojulikana kama 7 continental Races na zimeshawahi kupata tuzo mbalimbali za kimataifa.

Ujio wa mcheza sinema huyu aliyecheza sinema nyingi kama vile Santorini Blue, Perfect Strangers, The Great Fight, na nyingine nyingi unaiweka Tanzania katika macho ya dunia na kuwavutia watalii wengi kutoka taifa hili tajiri duniani. Deidre Lorenz alizaliwa katika jiji la Oregon nchini Marekani lakini akahamia katika jiji la New York City linalijulikana kama "The Big Apple" nchini Marekani akiwa na kampuni yake ya kutengeneza sinema inayoitwa Thira Films LLS.

eidre Lorenz ameshawahi kuteuliwa zaidi ya mara tatu kugombe tuzo za wacheza sinema maarufu duniani zinazojulikana kama Grammy Awards. Mcheza sinema huyu ataambatana na Wamarekani wengine kuja nchini tarehe 21 Juni kukimbia mbio hizi ambazo zimetokea kuutangaza sana mji wa Moshi tangu mwaka 1991. Lorenz alipatikana katika bahati nasibu iliyochezwa wakati wa mbio za New York Marathon mwaka jana.

Naye mwanzilishi wa mbio hizi mama Marie Frances ana historia ya kuanzisha mbio na matamasha mbalimbali duniani. Alikuwa pia mwanzilishi wa mbio za Pyramid Marathon nchini Misri pamoja na Miss Universe Egypt matamasha yaliyojizolea sifa kemkem.Aliombwa kuja kuanzisha mbio za Marathon nchini Tanzania na balozi wa Tanzania wa wakati ule nchini Misri.Mbio za Mt. Kilimahjaro Marathon ni moja kati ya mbio tafauti za marathon zinazifanyika katika mji wa Moshi.

Mount Kilimanjaro Marathon zitaanzia Moshi Club mpaka Rau madukani na kurudi mara tatu ambazo zitakuwa kilimeta 42. Kutakuwa pia na mbio z akilometa 21, kilimeta 10 na kilometa 5 kwa watoto. Wakimbiaji hawahitaji kuwa na ujuzi wa kukimbia watu wote wanaweza kukimbia.

Saturday, June 16, 2012


Twiga Stars Yanyukwa Na Ethiopia 1-0 Uwanja Wa Taifa




Mchezaji wa timu ya Twiga Stars, Mawanahamisi Omary akiondoka na mpira kuelekea goli la timu ya Ethiopia huku mabeki wa timu hiyo wakiwania mpira huo katika mchezo wa kuwania kufuzu fainali za kombe la mataifa ya Afrika zitakazofanyika mwaka ujao, mchezo huo umefanyika kwenye uwanja wa Taifa wa Dar es salaam.





Wachezaji wa timu za wanawake wa Tanzania na Ethiopia wakiingia uwanjani tayari kwa kuanza mchezo. Chanzo: www.fullshangweblog.com

Vyombo vya Habari Vitumike Kuhamasisha Zoezi la Sensa -


Baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya Taifa ya Sensa kwa upande wa Zanzibar wakiendelea na Kikao chao Mjini Dodoma chini ya Mwenyekiti wa Kikao hicho Waziri Mkuu Mh. Mizengo Pinda.

Mwenyekiti wa Kamati ya Taifa ya Sensa Waziri Mkuu Mh. Mizengo Pinda akiwa na Mwenyekiti Mwenza Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Bazlozi Seif wakikiendesha Kikao cha Tatu cha Kamati hiyo katika Ukumbi wa Wizara inayosimamia Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mjini Dodoma.


NBA TALLEST PLAYER




Just about every professional basketball player can leap up in the air and slam dunk, but how many can throw it down while barely leaving their feet?

Only one player on planet earth is known to have such a skill, but he doesn't play in the NBA. The iconic Harlem Globetrotters employ this gargantuan.

Paul Sturgess is his name, "Tiny" is his nickname, but there isn't much that's small about this 7-foot-8, 325-pound mountainous man.


The pride of Loughborough, England, Sturgess played basketball at West Virginia's Mountain State University in part because he liked the gloomy weather and the mountainous geography reminded him of home.

In addition to being crowned the World's Tallest Professional Basketball Player by Guinness World Records, Sturgess is the proud owner of a viral Internet video. The clip, posted a few days ago, appears to show "Tiny" dunk with probably the worst vertical ever.
WASHIRIKI WA AFRICA GOSPEL MUSIC AWARD

Baadhi ya waimbaji waliongizwa katika kuwania tuzo tuzo malimbali za Africa gospel music awards zinazotarajiwa kutolewa tarehe 7 mwezi july mwaka huu huko jijini London nchini Uingereza.


Christina Shusho - Tanzania


Diana Hamilton - uk


Dena mwana DRC Kongo


Kefee - Nigeria

Tuesday, June 12, 2012

                      Queen Seon Deok (K-Drama) (2009)


    Queen Seon Deok (K-Drama) (2009)
  • Title : Queen Seon Deok (K-Drama) (2009)
  • Alternative Title(s) : 선덕여왕 (善德女王) / Seondeok Yeo Wang
  • Number of Episodes: 62
  • Date Aired (YYYY-MM-DD): 2009-May-25 to 2009-Dec-22
  • More Info: http://wiki.d-addicts.com/Queen_Seon_Deok
  • Summary: 
    Deokman was born a twin but was abandoned as a baby and sent to a place far away by her father, King Jinpyeong in order to protect her from being killed by an influenced royal court lady, Mishil who tries to snatch away the throne from the royal successor. Deokman was later brought back to the Silla palace, where she joined forces with her twin sister Princess Cheonmyong to oppose Mishil. However, Mishil devised sinister plans to have the two Silla princesses exiled from the kingdom, and in a secretive battle, Princess Cheonmyong was accidentally killed. But Princess Deokman shrewdly enlisted the help of General Kim Yusin and eliminated her archenemy Mishil. She then became Queen Seon Deok, the first female ruler of the Silla kingdom. This drama is about a story of a beautiful queen, who has to give up her love to save the people and thus, leaving behind many brilliant achievements.